} });
 

TANGAZO
Misikiti minane kufungwa Tunisia
Utawala nchini Tunisia unasema kuwa utafunga misikiti 80 katika kipindi cha wiki moja inayokuja kwa madai ya kuhubiri chuki na jihad.
null
Zaidi ya watalii 2500 kutoka Uingereza wametoroka na kurejea makwao
Hii ni kufuatia shambulizi lililofanyika kwenye hoteli moja hapo jana ambapo takriban watu 39 wengi wao wakiwa raia wa mataifa ya ulaya waliuawa na mwanamme mmoja aliyejifanya kuwa mtalii.
null
Asili mia kubwa ya wahasiriwa wa mkasa huo ni raia wa Uingereza
Wapiganaji wanaoshirikiana na wanamgambo wa Kundi la kiislamu la Islamic State wamesema kuwa wao ndio waliotekeleza shambulizi hilo.
null
Miili ya watalii ilikuwa imetapakaa ufukweni
Waziri mkuu nchini Tunisia Hanib Essid anasema kuwa misikiti hiyo ndio iliokuwa ikitumika kueneza propaganda na kuunga mkono ugaidi.
null
Waziri mkuu ametangaza kuwa misikiti hiyo ndiyo imekuwa ikihubiri Jihad
Hali ya usalama umeimarishwa maradufu katika maeneo mengi mjini Tunis na karibu na majengo yenye watalii wengi.
null
Mpiganaji mmoja alijifanya kuwa mtalii kabla ya kuwafyatulia risasi watalii ufukweni
Tayari wanajeshi wa akiba wameamrishwa kuripoti mara moja katika kambi za jeshi zilizoko karibu nao.

soma habar kilasiku kazi ya mikono yangu ni kuhakikisha unapata unachotaka +255 769 859 030 #ZAMU YAKO 2016

TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by TeachMaker

Post a Comment

 
Top