TANGAZO
Akihutubia
mamia ya wananchi katika mji wa vawa wilayani Mbozi, katibu mkuu wa
chama cha demokrasia na maendeleo, Chadema, Dk. Wilbrod Slaa amesema
kuwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini wako hatarini kupoteza haki yao ya
kidemokrasia ya kupiga kura, kwa kuwa baadhi yao wamejiandikisha kwenye
vituo wakati wakiwa vyuoni, lakini wakati wa kupiga kura vyuo hivyo
vtakuwa vimefungwa na wanafunzi watakuwa majumbani mwao.
Mwenyekiti
wa Chadema mkoa wa Mbeya, Joseph Mwachembe maarufu kwa jina la china
amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vya kuandikishia
wapiga kura ili wakajiandikishe, huku pia akiiomba tume ya taifa ya
uchaguzi kuongeza mashine za uandikishaji kwenye vituo ambavyo vina
msongamano mkubwa wa wananchi wanaokwenda kujiandikisha.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa Chadema kanda ya nyanda za juu kusini,
mchngaji Dk. Steven Simon Kimondo amesema kuwa monyoko mkubwa wa maadili
ndio ambao umeliingiza taifa kwenye matatizo makubwa ikiwemo ubadhirifu
wa mali za umma.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by TeachMaker
Post a Comment