TANGAZO
Safari ya mwisho ya ndege ya kwanza
inayotumia nishati ya miale ya jua kupaa angani, imetatizika kutokana na hali
mbaya ya hewa.
Ndege hiyo iliondoka mapema Jumapili asubuhi mashariki mwa
Uchina, katika safari ya siku sita kuelekea Hawahi, lakini safari hiyo
imesitishwa baada ya hali ya hewa kuwa mbaya ilipokuwa kwenye anga ya bahari ya
Pacific.
Wataalamu wa utabiri wa hali ya anga, wamemuomba rubani wa ndege
hiyo kusitisha kwa muda safari hiyo ili kuruhusu hali ya hewa kuwa shwari,
ndipo aendelee na safari yake.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by TeachMaker

Post a Comment