TANGAZO
Hatimaye
kilio cha wakulima wa Tumbaku cha kukwama kuuza tumbaku yao kimemalizika baada
ya msimu wa kuuza zao hilo kufunguliwa jumatano Juni 03 Mwaka huu katika mkoa
wa kitumbaku wa Kahama
Hali hiyo
imeelezwa leo mjini Kahama na mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika KACU Peter
Emmanuel kuwa msimu huo utafunguliwa siku hiyo ya Jumatano hali ambayo itaondoa
malalamiko ya wakulima hao kulalamikia kuchelewa kwa msimu huo
Emmanuel
amefafanua kuwa utaratibu wa uuzaji wa Tumbaku hiyo utakwenda kwa dola na sio
shilingi kama ilivyolipotiwa hivi karibuni na vyombo vya habari kuwa tumbaku
itauzwa kwa shilingi wakati pembejeo italipwa kwa dola
Mwenyekiti
huyo amesema utaratibu wa kwenye mkataba ni ule wa kuuzwa zao hilo kwa dola
sambamba na pembejeo hiyo kulipwa kwa dola hali ambayo itawanufaisha wakulima
wa zao hilo kutokana na kupanda kwa fedha hiyo ya kigeni
Kabla ya
hapo meneja wa bodi ya tumbaku Tanzania wilayani Kahama Albert Challe amesema tatizo
la ucheleweshwaji wa ufunguzi wa msimu huo ulisababishwa na serikali
kuchelewesha kuleta fedha za kuendeshea zoezi hilo
Katika
msimu wa mwaka huu jumla ya kilo milioni 8 zinatarajiwa kuuzwa kwenye makampuni
mbalimbali ya ununuzi wa zao hilo hali ambayo inaweza kubadili kiuchumi, maisha
ya wakulima hao.
TANGAZO
Facebook Blogger Plugin by TeachMaker

Post a Comment